Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 16, 2024 Local time: 15:20

Uchumi wa Sudan unazidi kudidimia, benki ya taifa yasema


Raia wakiandamana dhidi ya mapinduzi ya kijeshi ya mwaka jana, mjini Khartoum. Picha ya AP, Februari 14, 2022.
Raia wakiandamana dhidi ya mapinduzi ya kijeshi ya mwaka jana, mjini Khartoum. Picha ya AP, Februari 14, 2022.

Uchumi wa Sudan kwa mara nyingine umedidimia baada ya mapinduzi ya kijeshi ya mwezi Oktoba, huku mauzo yake yakiporomoka kwa asilimia 85 kulingana na benki ya taifa, nayo sarafu yake ikipoteza thamani kwenye soko la magendo.

Kutokana na kusimamishiwa kwa misaada kutoka nje ya mabilioni ya dola, serikali inayoongozwa na wanajeshi ilipandisha bei na kodi kwenye kila kitu kuanzia huduma za afya hadi mafuta ya kupikia, ongezeko la bei ambalo limewakera sana wanainchi,

Mzozo wa kiuchumi wa Sudan wa muda mrefu, uliosababishwa na miongo kadhaa ya vita, kutengwa na vikwazo vya kiuchumi, ulionyesha dalili za afueni kabla ya mapinduzi, sasa leo umekuwa tishio kubwa la mzozo mpya wa kibinadamu, wakati wanainchi wake wanakabiliwa na machafuko mengine na ongezeko la viwango vya njaa.

Viongozi wa kijeshi wameshindwa kumteua waziri mkuu na maandamano yamepamba moto kwa miezi kadhaa.

Amin Shibeika ambaye ni mmiliki wa benki mjini Kharthoum anasema, mzozo wa kisiasa unaathiri biashara

XS
SM
MD
LG