Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 09:02

Uchaguzi wa visiwa vya Solomon kucheleweshwa kwa miezi 7


Sehemu ya mji mkuu wa visiwa vya Solomon wa Honiara
Sehemu ya mji mkuu wa visiwa vya Solomon wa Honiara

Wabunge kwenye visiwa vya Solomon Alhamisi wamepiga kura ya kuchelewesha uchaguzi mkuu wa mwaka ujao hadi 2024, hatua ambayo wakosoaji wanasema ni sawa na mapinduzi, wakihofia kwamba huenda ikasababisha kuendelea kwa ghasia visiwani humo.

Waziri mkuu wa visiwa hivyo Manasseh Sogavare, amesema kwamba kucheleweshwa huko kwa uchaguzi kwa muda wa miezi 7, kunahitaji marekebisho ya kikatiba, na ni kwa sababau taifa hilo ni mwenyeji wa michezo ya kimataifa ya Pacific, mwaka ujao.

Amasema kwamba kufanya uchaguzi sambamba na michezo hiyo kutagharimu hela nyingi pamoja na kuzua changamoto za kiufundi. Hata hivyo kiongozi wa upinzani Mathew Wale amesema kwamba hatua hiyo inahujumu haki ya wananchi ya kupiga kura mwaka ujao.

Ameongeza kusema kwamba ni mbinu ya waziri mkuu ya kubaki madarakani zaidi ya muhula wake. Sagavare amesema kwamba waziri mkuu amesababisha aibu ya kieneo , kama taifa ambalo lipo tayari kukiuka katiba yake ili kuwa mwenyeji wa michezo ya wiki mbili kinyume na matakwa ya wananchi wake.

XS
SM
MD
LG