Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 05:00

Uchaguzi Marekani 2020 : Maandamano yazuka Marekani baada ya matokeo kuchelewa

Darzeni ya wafuasi wanaomuunga mkono Rais Donald Trump wamekusanyika katika miji mbali mbali nchini wakati matokeo ya uchaguzi yanapotangazwa wakitaka zowezi la kuhesabu kura kusitishwa.

Huku maelfu ya wanaomunga mkono mgombea urais wa chama cha demokratik wakiandamana kutaka zoezi hilo liendele hadi mwisho.

Wafuasi wa Rais Donald Trump na Makamu wa Rais wa zamani Joe Biden wakikusanyika katika vituo vya kupiga kura wakati matokeo ya uchaguzi yakitangazwa Jumatano, huku maelfu ya wakiandamana Yutaka kura zote zihesabiwe.

Wafuasi wa rais wanadai kusitishwa zowezi la kukusanya kura zilizowasili kwa nia ya posta baada ya siku ya uchaguzi.

Wafuasi wa Trump wakiimba "Sitisheni kuhisabu kura" mjini Detroit. Na wale walkout katika mji wa Phoenix wakisema "Acheni wizi".

Wafuasi wa Mdemokrat Joe Biden wanasema, "Hisabuni kura zote, hisabuni kila kura zilizopigwa."

Pandisha zaidi

Makundi

XS
SM
MD
LG