Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 13, 2025 Local time: 09:48

Tume ya Umoja wa Mataifa yamaliza muda wake Mali


Tume  ya Umoja wa Mataifa nchini Mali, Jumapili imemaliza muda wake wa kufanyakazi katika taifa hilo lenye mizozo, kwa kutimiza ahadi ya siku ya mwisho iliyokubaliwa ya Desemba 31, baada ya viongozi wa kijeshi kutoa amri ya kuondoka kwake.

Tume hiyo ya kuleta uthabiti ya Umoja wa Mataifa kwa Mali (MINUSMA) ilikuwepo nchini humo toka 2013, na kujiondoa kwake kunazusha hofu kwamba mapigano yatapamba moto baina ya jeshi la nchi hiyo na makundi ya wenye silaha.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amesema katika taarifa iliyochapishwa Jumapili kwamba MINUSMA imefikia ukomo wake katika muda uliokubaliwa wa Desemba 31.

Kiongozi huyo wa Umoja wa Mataifa, ameipongeza tume hiyo kwa kuchukua jukumu muhimu la kuwalinda raia, na kusaidia mchakato wa amani ya Mali, ambayo imedhoofishwa na ghasia za makundi yenye msimamo mkali na migogoro mingine.

Forum

XS
SM
MD
LG