Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Februari 07, 2025 Local time: 10:49

Tume ya uchaguzi ya Nigeria yandaa mazoezi ya kucheki alama za vidole kwa wapiga kura


Maafisa wa uchaguzi wakikagua kadi za kudumu za wapiga kura katika kituo cha usambazaji kabla ya uchaguzi wa Urais wa Februari 2023 huko Lagos, Nigeria, Jumatano, Januari 11, 2023
Maafisa wa uchaguzi wakikagua kadi za kudumu za wapiga kura katika kituo cha usambazaji kabla ya uchaguzi wa Urais wa Februari 2023 huko Lagos, Nigeria, Jumatano, Januari 11, 2023

Tume ya uchaguzi ya Nigeria siku ya Jumamosi waliandaa  mazoezi ya kucheki alama za vidole kwa wapiga kura kabla ya uchaguzi wa rais na bunge mwezi huu.

Raia wa Nigeria watapiga kura Februari 25 kumchagua mrithi wa Rais Muhammadu Buhari ambaye ataachia madaraka baada ya mihula miwili madarakani inayoruhusiwa kikatiba.

Magavana wa majimbo na wabunge watachaguliwa wiki mbili baadaye.

Nigeria, taifa lenye watu wengi zaidi barani Afrika na lenye uchumi mkubwa sana, lina historia ndefu ya kasoro wakati wa uchaguzi, udanganyifu na ghasia.

Buhari, jenerali wa zamani wa jeshi mwenye umri wa miaka 79, ameahidi uchaguzi ulio huru na wa haki.

Ili kukuza haki, uaminifu na uwazi wa mchakato wa uchaguzi, Tume Huru ya Kitaifa ya Uchaguzi (INEC) ilianzisha mfumo wa kuidhinisha wapiga kura katika kura za mwaka 2015 na 2019.

Lakini mfumo huo uligubikwa na mapungufu.

XS
SM
MD
LG