Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:00

Trump: 'Marekani itauchukua Ukanda wa Gaza na tutaifanyia kazi' 


Rais wa Marekani Donald Trump (kulia) akimsikiliza Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa East Room wa White House Washington, DC, on Februari 4, 2025.
Rais wa Marekani Donald Trump (kulia) akimsikiliza Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa East Room wa White House Washington, DC, on Februari 4, 2025.

Rais Donald Trump wa Marekani amesema anataka  Marekani ichukue umiliki wa Gaza ikiwa ni msimamo baada ya  taarifa zake za awali za kuwalazimisha wakazi wa Gaza kuhamishiwa nchi jirani za Jordan na Misri.

Trump alitoa tangazo hilo la kushangaza Jumanne jioni baada ya kukutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu huko White House.
Wakati maelfu ya wakazi wa Gaza wakirudi katika nyumba zao zilizobomolewa kufuatia makubaliano ya sitisho la mapigano la Januari 19 kati ya Israel na Hamas, Rais Trump siku ya Jumanne alitoa tangazo la kushangaza.


Donald Trump, Rais wa Marekani: "Marekani itauchukua Ukanda wa Gaza na tutaifanyia kazi."
Matamshi hayo ya Trump yanavuka yale aliyosema mwezi uliyopita kwamba atawahamisha wakazi wa Gaza hadi nchi jirani za Jordan na Misri.

Anasema anataka kujenga eneo hilo kuwa alichokiita “mandhari ya Kitalii ya Riviera katika Mashariki ya Kati.

Ismael Mohammed, miaka 47, na familia yake, waliokoseshwa makazi upande wa kusini mwa Gaza wakiwa njiani kurejea katika nyumba zao zilizoharibiwa kabisa wakati ambapo sitisho la mapigano kati ya Hamas na Israel likiendelea, huko Gaza City, Januari 28, 2025.
Ismael Mohammed, miaka 47, na familia yake, waliokoseshwa makazi upande wa kusini mwa Gaza wakiwa njiani kurejea katika nyumba zao zilizoharibiwa kabisa wakati ambapo sitisho la mapigano kati ya Hamas na Israel likiendelea, huko Gaza City, Januari 28, 2025.

Donald Trump, Rais wa Marekani kila mtu niliyezungumza naye amelipenda wazo la Marekani kumiliki eneo hilo, kulijenga na kubuni maelfu ya nafasi za ajira, na kulibadili kuwa la kuvutia ambalo hakuna atakayelitambua.

Hakuna mtu anayetaka kuliangalia kwasababu wanachoona ni vifo na uharibifu na vifusi.
Trump alitoa tangazo hilo baada ya kumkaribisha Waziri mkuu wa Israel Benjamina Netanyahu huko White House.
Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel: "Nimesema hili hapo kabla. Ninasema tena Wewe ndiye rafiki mkubwa wa Israel kuwahi kuwepo hapa White House."
Trump hakufafanua jinsi anavyopanga kuchukua udhibiti wa Gaza eneo ambalo limeharibiwa na miezi 15 ya vita. Hakufuta uwezekano wa kupeleka wanajeshi wa Marekani. Haiko bayana kuikalia Gaza kutaingiliana vipi na lengo la Trump mwenyewe la kupanua mkataba wa Abraham kuihusisha Riyadh. Mkataba ambao aliousimamia ambao ulianzisha uhusiano kati ya Israel na nchi za Kiarabu mwaka 2020.

Mnamo Machi 14, 2017 wakati Rais wa Marekani Donald Trump Qatar alipokutana na Waziri wa Ulinzi na Mwana Mfalme Mrithi Mohammed Bin Salman wakiwa Oval Office, White House.
Mnamo Machi 14, 2017 wakati Rais wa Marekani Donald Trump Qatar alipokutana na Waziri wa Ulinzi na Mwana Mfalme Mrithi Mohammed Bin Salman wakiwa Oval Office, White House.

Saudi Arabia imesema itakubali kuitambua Israel ikiwa tu vita vya Gaza vinamalizika na Wapalestina wanapata taifa lao.
Mirette Mabrouk, Taasisi ya Mashariki ya Kati anasema: "Kuwahamisha Wapalestina kwenda mataifa jirani sio mwanzo mzuri, kwa hivyo ninadhani itakuwa na athari kubwa, zaidi ya hapo hatujui, mambo yatakavyo kuwa na Rais Trump, itatubidi tusubiri tuone."
Tangazo la trump kuhusu Gaza ni ishara yake ya karibuni ya dhamira ya upanuzi, kufuatia taarifa zake za awali za kuichukua Greenland kutoka Denmark, kuuchukua Mfereji wa Panama na kuiunganisha Canada na Marekani.
Kabla ya mkutano wake na Netanyahu, Trump aliamuru kurudisha tena kampeni yake ya kuishinikiza Iran ili kuizuia kupata silaha ya nyuklia. Vile vile alisitisha misaada kwa shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya wakimbizi wa Palestina na kuiondoa Marekani kutoka baraza la haki za Bindamu la Umoja wa Mataifa ambayo anasema inachukia Wayahudi.

Forum

XS
SM
MD
LG