Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 18, 2025 Local time: 17:05

Trump alinyooshea kidole jeshi la Marekani kwa "Drone"


Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump
Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump

Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, Jumatatu amelilaumu jeshi la nchi, akidai linaficha kuhusu ndege zisizo na rubani zisizo na taarifa kamili zinazoruka usiku mashariki mwa Marekani, hata hivyo Pentagon ilikanusha mara moja madai yake. 

Trump alisema jeshi linajua, na kwamba kuna jambo la ajabu linaendelea, akiwaambia waandishi wa habari akiwa Mar-a-Lago, Florida katika mkutano wake wa kwanza na wanahabari toka achaguliwe kwa muhula mpya wa miaka minne unaoanza mwakani.

Baada ya Trump kuzungumza, Meja Jenerali wa jeshi la anga Pat Ryder, msemaji wa Pentagon, aliwaambia wanabari kwamba hakuna ushahidi kwa sasa kwamba kuonekana huko kwa ndege zisizo na rubani ni tishio la usalama wa taifa, umma, au kuwa kuna kuingiliwa na mataifa ya kigeni.

Forum

XS
SM
MD
LG