Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Juni 18, 2025 Local time: 15:08

Tetemeko la ardhi latikisa jiji la New Jersey na New York


Katika picha hii huu, simu inaonyesha ujumbe wa Tahadhari ya Dharura siku ya Aprili 5, 2024, ikionya kuhusu tetemeko la ardhi huko New York. AFP.
Katika picha hii huu, simu inaonyesha ujumbe wa Tahadhari ya Dharura siku ya Aprili 5, 2024, ikionya kuhusu tetemeko la ardhi huko New York. AFP.

Maafisa wanasema tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 4.7 vipimo vya rikta lilitikisa eneo la jiji lenye watu wengi la New York City. Wakazi waliripoti kuwa walihisi kunguruma kote kaskazini mashariki siku ya Ijumaa asubuhi.

Tetemeko hilo lilitokea katikati ya Lebanon, New Jersey, au takriban maili 45 magharibi mwa Jiji la New York na maili 50 kaskazini mwa Philadelphia.

Idara ya Zimamoto ya New York inasema hakuna ripoti za awali za uharibifu. Msururu wa msongamano wa magari katikati ya jiji la Manhattan uliongezeka zaidi huku madereva wakipiga honi kwenye mitaa iliyokuwa ikikumbana na tetemeko.

Baadhi ya wakazi wa Brooklyn walisikia kelele kubwa na kuhisi jengo lao likitikisika. Watu huko Baltimore, Philadelphia, Connecticut na maeneo mengine ya Pwani ya Mashariki pia waliripoti kusikia tetemeko.

Gavana wa New York Kathy Hochul aliandika kwenye X kwamba tetemeko hilo lilisikika katika jimbo lote. "Timu yangu inatathmini athari na uharibifu wowote ambao unaweza kuwa umetokea, na tutasasisha umma siku nzima," Hochul alisema.

Forum

XS
SM
MD
LG