Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 12:11

Takriban watu 20 wafariki katika ajali ya moto New York


Takriban watu 20 wafariki katika ajali ya moto New York
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:09 0:00

Watu 19 wakiwemo watoto 9 wamekufa Jumapili kutokana na moto kwenye kitongoji ya Bronx mjini New York, ukiwa mkasa uliolezewa kuwa mbaya zaidi na mkuu wa zima moto mjini humo katika miaka ya karibuni.

Mshauri mkuu wa meya wa New York Eric Adams Jumapili amedhibitisha vifo hivyo wakati afisa mmoja wa jiji ambaye hakuruhusiwa kuzungumza hadharani akidhibitisha vifo vya watoto.

Darzeni ya watu pia wanasemekana kujeruhiwa wakati wa moto huo,13 miongoni mwao wakisemekana kuwa katika hali mahututi. Idara ya moto ya New York imesema kwamba zaidi ya wazima moto 200 walishiriki kuzima moto huo kwenye nyumba za makazi za Twin Park.

XS
SM
MD
LG