Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 09:41

Takriban nusu ya nchi zote duniani zashuhudia kuzorota demokrasia -Ripoti


Ripoti ya Freedom House 2023 kuhusu haki za kisiasa na uhuru wa kiraia. (Courtesy Photo: Freedom House)
Ripoti ya Freedom House 2023 kuhusu haki za kisiasa na uhuru wa kiraia. (Courtesy Photo: Freedom House)

Karibu nusu ya nchi zote duniani zinashuhudia kushuka kwa viwango vya demokrasia.

Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya masuala ya kigeni ya Baraza la Wawakilishi kuhusu Afrika, Afya ya Kimataifa , Haki za Binadamu za Kimataifa , na Jumuiya za Kimataifa Christopher Smith (kulia) akiongea na Kiongozi msaidizi wa Ofisi ya Demokrasia Nancy Lindborg, nchini Marekani.
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya masuala ya kigeni ya Baraza la Wawakilishi kuhusu Afrika, Afya ya Kimataifa , Haki za Binadamu za Kimataifa , na Jumuiya za Kimataifa Christopher Smith (kulia) akiongea na Kiongozi msaidizi wa Ofisi ya Demokrasia Nancy Lindborg, nchini Marekani.

Hii ni kulingana na ripoti ya shirika la kimataifa la kufuatilia demokrasia iliyotolewa leo Alhamisi.

Kulingana na ripoti hiyo, baadhi ya nchi ambazo zimekuwa zikitambuliwa kuheshimu demokrasia, pia zimejiunga katika orodha ya nchi ambazo viwango vya demokrasia vimeshuka.

Taasisi ya demokrasia na msaada wa uchaguzi IDEA, yenye makao yako Stockholm, Sweden, imesema kwamba viwango vya demokrasia katika nchi 85 kati ya 173 zilizohusishwa katika utafiti huo vimeshuka katika muda wa miaka 5 iliyopita.

Ubaguzi nchini Marekani, ukandamizaji wa uhuru wa waandishi wa habari nchini Austria, na upatikanaji wa haki nchini Uingereza ni miongoni mwa mambo ambayo yametajwa kushuka katika utafiti huo.

Viwango vya demokrasia pia vimeshuka Hungary, Peru na nchi za Afrika ambapo viwango hivyo vimeshuka sana kutokana na mapinduzi ya kijeshi.

Forum

XS
SM
MD
LG