Marekani imelaani vikali shambulizi la anga dhidi ya Sudan Kusini kwenye vinu vya mafuta yaliyofanywa na jirani zao Sudan. Katika taarifa Alhamisi msemaji wa wizara ya mambo ya nje Victoria Nuland alisema mashambulizi kama hayo kwa maeneo ya raia ni mabaya. Amesema Marekani inaitaka serikali ya Sudan kuacha mashambulizi ya anga ambayo anasema yanavunja sheria ya kimataifa. Msemaji wa jeshi la Sudan Sawarmi Khaled Saad amekanusha kuwa nchi yake ilihusika na mashambulizi hayo ya mabomu.