Stoltenberg ameambia mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi wanachama kwamba NATO ipo tayari kukaribisha uanachama wa Ukraine.
Mkutano huo umefanyika Romania, kujadili namna ya kuendelea kutoa msaada wa silaha kwa Ukraine. Ukraine ilituma maombi ya kutaka kujiunga na NATO mara kwanza mwaka 2018.
Amesema kwamba North Macedonia na Montenegro wamejiunga na muungano huo ulioanzishwa baada ya vita vya pili vya dunia, na kwamba Sweden na Finland zitajiunga hivi karibuni, akisisitiza kwamba Russia haina uwezo wowote wa kuzuia nchi hizo kujiunga na NATO.
Stoltenberg amesema kwamba rais Viladimir Putin hana uwezo wowote wa kuzuia nchi zenye uhuru wake kufanya maamuzi yake na ambayo sio tishio kwa usalama wa Russia na kwamba Putin anaogopa ukuaji wa demokrasia na uhuru wa nchi.