Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 23:54

Shirika la ndege la Kenya Airways kuathiriwa na uhaba wa vipuri vya ndege


Ndege ya shirika la Kenya Airways
Ndege ya shirika la Kenya Airways

Shirika la ndege la Kenya la Kenya Airways, limewaambia  wateja wake kuhusu  uwezekano wa kuvurugika kwa baadhi ya safari zake wakati wa msimu wa sikukuu ya  Krismasi kutokana na uhaba wa vipuri.

Shirika hilo ambalo ni moja ya mashirika makubwa sana ndege barani Afrika, limesema kwamba uhaba huo ambao unashuhudiwa kote ulimwenguni utaathiri safari zake kwa takriban wiki mbili.

Taarifa ambayo Reuters imeiona leo Jumatatu imesema kwamba, “Changamoto zilizopo zitaongeza muda wa ukarabati wa ndege zetu, wakati pia zikipelekea kusitishwa kabisa kwa safari za ndege moja au mbili.”

Mara ya kwanza Kenya Airways kulalamikia uhaba wa vipuri ilikuwa Januari mwaka huu, wakati huo ikelezea kuwa uhaba huo umetokana na vita vya Ukraine ambavyo vilizuia mfumo wa usambazaji wa Russia kwa sekta ya anga ulimwenguni.

Forum

XS
SM
MD
LG