Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 19:46

Shambulizi limeua 26 Pakistan


Watu wakitembea kwenye mabaki ya kituo cha treni mjini Quetta, Pakistan. Nov 9 2024
Watu wakitembea kwenye mabaki ya kituo cha treni mjini Quetta, Pakistan. Nov 9 2024

Mlipuaji wa kujitoa mhanga amejilipua katika kituo cha reli chenye watu wengi katika jimbo la Balochistan liloshudhuia ghasia kusini magharibi mwa Pakistan.

Mlipuko umeua watu 26 na kujeruhi wengine 60.

Afisa wa ngazi ya juu wa polisi Mohammad Baloch amewaambia waandishi wa habari kwamba mlipuko mkubwa katika mji mkuu wa Quetta ulitokea katika sehemu ya abiria kusubiri treni na kwamba sehemu hiyo ilikuwa na karibu watu 100 wakati wa tukio.

Karibu nusu ya waliofariki na wengi wa waliojeruhiwa ni wanajeshi wa Pakistan, ambao inaaminika ndio waliokuwa wamelengwa katika shambulizi hilo.

Msemaji wa serikali ya jimbo Shahid Rind, amesema kwamba watu 10 kati ya waliojeruhiwa wapo katika hali mahututi.

Kundi la wapiganaji la Baloch, limedai kuhusika na shambulizi hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG