Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 20, 2025 Local time: 14:06

Shambulizi la Russia laua 14 Ukraine


Shambulizi la Russia, kwenye  duka la vifaa vya ujenzi DIY lililokuwa na msongamano  mkubwa wa watu mjini Kharkiv limeuwa watu 14 na wengine kadhaa wamejeruhiwa, maafisa wa Ukraine wamesema Jumapili asubuhi.

Idadi ya waliofariki dunia inaongezeka katika jiji la pili kwa ukubwa nchini humo wakati lilikumbwa na mashambulizi mawili siku moja iliyopita.

Mabomu mawili yaliyolenga hapo yaliharibu duka la DIY katika eneo la makazi ya jijini humo Jumamosi mchana, Gavana wa mkoa Oleh Syniehubov, alisema kwenye televisheni ya taifa.

Mashambulizi hayo yalisababisha moto mkubwa ambao na moshi mzito mweusi ulisambaa mamia ya mita angani.

Watu 43 walijeruhiwa ofisi ya waendesha mashtaka wa eneo imesema. Meya wa Kharkiv, Ihor Terekhov amesema takriban watu 120 walikuwepo katika duka la vifaa wakati mabomu yalipolipuka.

Forum

XS
SM
MD
LG