Shakira, mwenye umri wa miaka 45, anaamini kuwa hana hatia na anachagua kuliaciha suala hilo mikononi mwa sheria, kampuni ya mahusiano ya umma ya Llorente y Cuenca (Yorente Kuenka) ilisema katika taarifa yake.
Waendesha mashtaka wa Uhispania walimshtaki mwimbaji huyo mwaka 2018 kwa kutolipa ushuru wa euro milioni 14.5 kwa mapato yaliyopatikana kati ya 2012 na 2014.
Anakabiliwa na uwezekano wa kutozwa faini na kifungo, iwapo atapatikana na hatia ya kukwepa kodi.
Hakuna maelezo ya haraka yaliyopatikana kutoka kwa waendesha mashtaka juu ya mpango huo. Hakuna tarehe ya kesi iliyopangwa.