Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 13:00

Serikali ya Marekani yaishtaki Google kwa kukiuka sheria ya biashara ya mtandaoni


Mwanasheria mkuu wa Marekani Merrick Garland
Mwanasheria mkuu wa Marekani Merrick Garland

Wamesema wamewasilisha malalamiko mahakamani kwa lengo la kumaliza ukiritimba wa kampuni hiyo kwenye mfumo mzima wa matangazo ya mtandaoni, ambao unaathiri vibaya watangazaji, wanunuzi na serikali ya Marekani.

Serikali inadai kuwa mpango wa Google wa kutaka kutawala katika matangazo ya mtandaoni, umekuwa wa kudhibiti au kuondoa wapinzani kupitia ununuzi na kulazimisha watangazaji kutumia bidhaa zake kwa kufanya iwe vigumu kutumia bidhaa za washindani wake.

Shauri hilo liliwasilishwa katika mahakama ya serikali kuu mjini Alexandria, Virginia.

XS
SM
MD
LG