Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 15:36

Serikali ya Guinea yauvunja muungano mkubwa wa upinzani


Kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Guinea Mamadi Doumbouya akiapishwa kama rais wa mpito mjini Conakry, Oktoba 1, 2021. Picha ya Reuters
Kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Guinea Mamadi Doumbouya akiapishwa kama rais wa mpito mjini Conakry, Oktoba 1, 2021. Picha ya Reuters

Serikali ya Guinea iliyoteuliwa na jeshi imelivunja vuguvugu la upinzani nchini humo, lijulikanalo kama National Front for the Defence of the Constitution (FNDC), chini ya amri iliyothibitishwa na shirika la habari la AFP Jumanne.

Muungano huo unaojumuisha vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi na mashirika ya kiaraia, uliongoza maandamano dhidi ya rais wa zamani Alpha Conde kabla ya kuondolewa kwake madarakani katika mapinduzi ya kijeshi mwaka jana.

Mvutano umekuwa ukiongezeka kwa miezi kadhaa kati ya FNDC na utawala wa kijeshi, na kuibua katika taarifa ya muungano huo siku ya Jumatatu ukisema kwamba utafanya maandamano Agosti 17.

Amri hiyo ya Jumamosi, iliyosainiwa na waziri wa utawala wa ndani Mory Conde ikitangaza kuvunjwa kwa FNDC, imethibitishwa na AFP Jumanne.

“Kundi hilo lililojiteua linaloitwa FNDC, limevunjwa kuanzia tarehe ya kutiwa saini amri hii,” uamuzi huo umesema.

Amri hiyo imesema” FNDC kwa kuendesha harakati zake inajihusisha na mashambulizi mabaya yanayofanywa wakati wa maandamano yaliyopigwa marufuku, mashambulizi dhidi ya watu wasiokubaliana na itikadi yao, na mashambulizi yanayolenga maafisa wa usalama.”

XS
SM
MD
LG