Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 18, 2025 Local time: 04:01

Serikali wa waziri mpya yatangazwa Morocco


Mkimbizi nchini Morocco akitafuta chakula kwenye taka
Mkimbizi nchini Morocco akitafuta chakula kwenye taka

Mfalme wa Morocco Mohammed wa sita Alhamisi ametangaza serikali mpya inayoongozwa na Aziz Akhannouch, tajiri billionea alie karibu na kasri, ambaye atakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi yaliyoongezeka kutokana na janga la virusi vya corona.

Baraza hilo lenye mawaziri 24 ambalo limeundwa baada ya chama cha watu huru cha Akhannouch RNI kuwashinda waislamu walio madarakani katika uchaguzi mwezi uliopita, lina wanawake saba, wakati utawala uliopta ulikuwa na mawaziri wanawake wanne.

Serikali hiyo inaundwa kwa kiasi kikubwa na watu wenye taaluma wasioegemea vyama vya siasa, pamoja na mwanadiplomasia mkongwe Nasser Bourita ambaye ameshikilia nafasi yake kama waziri wa mambo ya nje, katika hali ya mivutano ya kikanda, haswa na nchi jirani ya Algeria.

XS
SM
MD
LG