Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 17, 2025 Local time: 14:57

Sera ya Uingereza kuwapeleka wahamiaji Rwanda ni halali-Mahakama kuu ya London


Waandamanaji wakishikilia mabango nje ya kituo cha kufurusha wahamiaji karibu na uwanja wa ndege wa Gatwick, kusini mwa London, wakipinga mpango wa Uingereza kuwapeleka waomba hifadhi Rwanda. Juni 12, 2022. Picha ya AFP
Waandamanaji wakishikilia mabango nje ya kituo cha kufurusha wahamiaji karibu na uwanja wa ndege wa Gatwick, kusini mwa London, wakipinga mpango wa Uingereza kuwapeleka waomba hifadhi Rwanda. Juni 12, 2022. Picha ya AFP

Mpango wa Uingereza wa kuwapeleka wahamiaji nchini Rwanda ni halali, Mahakama kuu ya London imeamua leo Jumatatu, lakini imeridhia changamoto za kisheria za waomba hifadhi wanane.

Sera hiyo ambayo ilitangazwa mwezi Aprili, itairuhusu Uingereza kupeleka maelfu ya wahamiaji huko Rwanda ambao huwasili kwenye mwambao wake kutoka zaidi ya kilomita 6,400.

Akitangaza uamuzi wa mahakama hiyo, jaji Clive Lewis amesema ni halali kwa Uingereza kufanya mipango na serikali ya Rwanda kuwapeleka waomba hifadhi nchini humo na maombi yao ya kupewa hifadhi yataamuliwa huko.

Amesema “Katika mazingira hayo, kuhamishwa kwa waomba hifadhi nchini Rwanda kunaheshimu mkataba wa wakimbizi na majukumu mengine ya kisheria kwa serikali, likiwemo jukumu lililowekwa na sheria ya haki za binadamu ya mwaka 1998.”

Lakini jaji huyo amesema, waziri wa mambo ya ndani, waziri wa usalama lazima wazingatie ipasavyo mazingira “ya maombi ya kila mtu binafsi.”

XS
SM
MD
LG