Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 15, 2025 Local time: 00:47

Senegal: Mwanahabari mashuhuri aliye katika mgomo wa kula alazwa hospitali


Rais wa Senegal Macky Sall akihutubia mkutano wa 77 wa Baraza kuu la Umoja wa mataifa, kwenye makao makuu ya UN, Septemba 20, 2022
Rais wa Senegal Macky Sall akihutubia mkutano wa 77 wa Baraza kuu la Umoja wa mataifa, kwenye makao makuu ya UN, Septemba 20, 2022

Pape Ale Niang, mwandishi wa habari mashuhuri na mkosoaji wa serikali ya Senegal ambaye amekuwa katika mgomo wa kula kupinga mashtaka yanayomkabili, alipelekwa hospitali, wakili wake ameiambia AFP Jumapili.

Niang alipelekwa hospitali Jumamosi jioni baada ya afya yake kuzorota kama matokeo ya mgomo wake wa njaa wa hivi karibuni, amesema Moussa Sarr, mmoja wa mawakili wake.

Katika kesi iliyozusha wasiwasi wa kimataifa, Niang alikamatwa tarehe 6 Novemba na kushtakiwa kwa kufichua habari zinazoweza kuhujumu ulinzi wa taifa.

Alianza mgomo wa kula tarehe 2 Disemba na alipelekwa baadaye kwenye hospitali baada ya afya yake kuzorota.

Aliachiliwa kwa muda lakini alikamatwa tena baadaye tarehe 20 Disemba, ambapo alianza mgomo mwingine wa kula.

Niang, mkurugenzi wa gazeti la mtandaoni Dakar matin, ana wafuasi wengi nchini Senegal kwa taarifa zake za mara kwa mara kuhusu habari zinazojiri nchini.

XS
SM
MD
LG