Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 19, 2025 Local time: 20:21

Saudia kupunguza uzalishaji mafuta kutokana na shambulizi la Wahuthi


Kikosi cha Zimamoto firefighters wakijaribu kuzima moto katika kituo cha uzalishaji wa mafuta cha Aramco mpakani na mji wa Jizan, Saudi Arabia, mapema Jumapili, Machi 20, 2022. (Saudi Press Agency via AP)
Kikosi cha Zimamoto firefighters wakijaribu kuzima moto katika kituo cha uzalishaji wa mafuta cha Aramco mpakani na mji wa Jizan, Saudi Arabia, mapema Jumapili, Machi 20, 2022. (Saudi Press Agency via AP)

Saudi Arabia ambayo ni mzalishaji na muuzaji mkubwa mafuta ghafi duniani imetangaza kupunguza kwa muda uzalishaji huo katika kiwanda chake kinachosimamiwa na kampuni kubwa ya mafuta ya Aramco baada ya waasi wa Kihuthi kuazisha mashambulizi mpakani.

Shambulizi lililotekelezwa na ndege isiyokuwa na rubani dhidi ya kiwanda cha kusafisha mafuta cha YASREF katika mji wa viwanda wa Yanbu karibu na bahari ya sharma limepelekea kupungua kwa uzalishaji wa mafuta.

Wizara ya Nishati imesema kwamba hakuna matu aliuawa katika shambulizi hilo.

Taarifa ya wizara ya nishati imesema kwamba mashambulizi mawili yaliyotekelezwa na ndege zisizokuwa na rubani, yaligonga viwanda vya Yanbu na YASREF, vinavyozalisha pipa 400,000.

Maafisa wamesema kwamba shambulizi hiyo linafuatia shambulizi kama hilo lililotekelezwa Jumamosi dhidi ya kiwanda cha kusambaza petrol katika mji wa Jizan, kusini mwa nchi hiyo.

Waasi wa Kihuthi, wanaoungwa mkono na Iran, na ambao wanapambana na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia nchini Yemen, wamekuwa wakitekeleza mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya ufalme huo ikiwemo dhidi ya viwanda vinavyosimamiwa na Aramco.

Habari hii inatokana na vyanzo mbalimbali vya habari.

XS
SM
MD
LG