Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 18:07

Saudi Arabia na Russia kupunguza zaidi uzalishaji wa mafuta mwezi Agosti


Kituo cha mafuta cha Khurais, Saudi Arabia
Kituo cha mafuta cha Khurais, Saudi Arabia

Saudi Arabia na Russia, wauzaji wakubwa wa mafuta duniani, Jumatatu zimetangaza kupunguza zaidi uzalishaji wa mafuta, na kusababisha bei ya bidhaa hiyo kupanda huku kukiwa na wasiwasi wa kudorora kwa uchumi wa dunia na uwezekano kwa benki kuu ya Marekani kuongeza kiwango cha riba.

Saudi Arabia imesema itapunguza uzalishaji wa mafuta kwa mapipa milioni moja kwa siku kwa kipindi cha mwezi mmoja mwingine ukiwemo mwezi wa Agosti, ikiongeza kuwa hatua ya kupunguza uzalishaji wa mafuta itaendelea baada ya Agosti.

Muda mfupi baada ya tangazo hilo la Saudi Arabia, naibu waziri mkuu wa Russia Alexander Novak amesema Moscow itapunguza mauzo ya nje ya mafuta yake kwa mapipa 500,000 kwa siku mwezi Agosti.

Kiwango kilichopunguzwa na nchi hizo mbili ni sawa na asilimia 1.5 ya mafuta yanayouzwa duniani na kufikia kiwango cha hadi mapipa milioni 5.16 kwa siku ambacho nchi zinazozalisha mafuta wanachama wa OPEC zilikuwa zimeahidi kupunguza.

Baada ya taarifa ya kupunguzwa kwa uzalishaji wa mafuta, bei ya mafuta ghafi kwenye soko la kimataifa imeongezeka kwa senti 89 hadi dola 76.30 kwa pipa moja.

Forum

XS
SM
MD
LG