Kuna wasiwasi kwamba uchaguzi huo huenda ukavuruga zaidi uhalali wa utawala huo huku imani kati ya raia wa Iran ikionekana kufifia.
Uchaguzi utafanyika Juni 28, kumchagua rais mpya baada ya kifo cha Ebrahim Raisi.
Uchaguzi huo utahitajika kuwaleta pamoja raia wa Iran ambao hawakuonyesha dhamira kubwa katika uchaguzi wa mwaka 2021 uliopelekea Raisi kuingia madarakani.
Idadi kubwa ya wapiga kura wamekuwa hawashiriki katika uchaguzi mkuu katika jamhuri hiyo ya kiislamu.
Kulingana na wachambuzi, raia wa Iran wana wasiwasi kuhusu uchumi wa taifa, na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza.
Forum