Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 07:48

Serikali Afrika Kusini kukata rufaa kwa kesi ya mwanariadha Pistorius


Olympic and Paralympic track star Oscar Pistorius leaves court after appearing for the 2013 killing of his girlfriend Reeva Steenkamp in the North Gauteng High Court in Pretoria, South Africa, June 14, 2016.
Olympic and Paralympic track star Oscar Pistorius leaves court after appearing for the 2013 killing of his girlfriend Reeva Steenkamp in the North Gauteng High Court in Pretoria, South Africa, June 14, 2016.

Kiongozi wa mashtaka nchini Afrika ya Kusini amesema kuwa afisi yake ina mpango wa kukata rufaa kupinga kifungo cha miaka sita kilichotolewa na mahakama kwa mwanariadha Oscar Pistorius, na kudai kuwa mahakama haikutoa kifungo kilichostahiki.

Pistorius alihukumiwa kifungo cha miaka sita mapema mwezi huu baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp miaka mitatu iliyopita.

Kifungo hicho kilipunguza kutoka miaka kumi na mitano ambacho ndio muda mfupi sana unaotambuliwa na sheria za nchi hiyo. Katika kupunguza kifungo hicho, jaji Thokozile Masipa alisema kuwa mshtakiwa alionekana kuhuzunika na kuwa tayari alikuwa ametumika muda mrefu kwenye jela. Aliongeza kuwa Pistorius hakuwa amevaa mguu wake bandia wakati alipotekeleza mauaji hayo.

XS
SM
MD
LG