Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 29, 2023 Local time: 19:30

Rwanda yasikitishwa na Ubelgiji kukataa kumuidhinisha balozi wake


Rwanda Genocide Anniversary Kagames Leadership

Rwanda inachukulia hatua ya Ubelgiji kukataa kuidhinisha uteuzi wa balozi wake kama jambo la kusikitisha msemaji wa serikali ya Rwanda alisema Jumatano, akiongeza kuwa hatua hiyo haina ishara nzuri kwa uhusiano wa nchi hizo mbili.

Vincent Karega balozi wa zamani wa Rwanda nchini Afrika Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambako alifukuzwa Oktoba mwaka jana katikati ya mvutano kati ya nchi hizo mbili alichaguliwa na mamlaka mjini Kigali kuwa balozi nchini Ubelgiji.

Inasikitisha kwamba serikali ya Ubelgiji inaonekana kuwa imekubali shinikizo kutoka kwa serikali ya DRC na propaganda kutoka kwa mashirika na wanaharakati wanaopinga alisema msemaji wa serikali ya Rwanda Yolande Makolo.

Hii haijakaa vyema kwa mahusiano ya pande mbili baina ya nchi zetu.

Forum

XS
SM
MD
LG