Msemaji wa jeshi la Jamhuri ya Kedomkrasia ya Congo katika eneo la Kivu Kaskazini amesema ameshangaa kuona Jeshi la Rwanda likiingia nchini humo kwa zaidi ya kilomita moja jumamosi bila taarifa yoyote.
Wanajeshi hao waliingia hadi Banagana Buhumba eneo lililoko kilomita 32 kaskazini mwa Goma. Kapteni Djike Kaiko Guyom amesema tabia hiyo ni ya uchokozi na imetokea kwa mara ya pili jambo ambalo jeshi lake halitakubali tena.
Mwishoni mwa Juma, watu wenye silaha walishambulia kambi moja magharibi mwa Rwanda ambapo Rwanda ilidai ni waasi wa FADLR kutoka DRC.
Zikiliza ripoti zaidi kutoka kwa Austele Malivika akiwa Buhumba.