Baada ya makamu wa Rais wa Kenya William Ruto kuondolewa mashitaka yaliokuwa yanamkabili mbele ya mahakama ya ICC akiwa pamoja na mtangazaji wa Radio Joshua arap Sang, maswali mengi yameibuka hasa miongoni mwa wakenya.
Harrison Kamau ameweza kuzungumza na mchambuzi wa maswala ya kisiasa kutoka Kenya Bw Patrick Ochieng' na akataka kujua kama hali ya kisiasa itaathiriwa na hatua hiyo. Wengi kwa hakika wamefurahishwa na tangazo hilo lakini kuna wale waathirika wa mapigano ya kikabila yaliotokea nchini humo ambao wangali wanangojea haki ifanyike kwa upande wao. Zikiliza mahojiano.