Balozi Vasyl Bodnar, amesema kwamba Russia inasafirisha nafaka iliyoibwa kutoka Ukraine, na kuongezea kwamba utawala wa Kyiv unashirikiana na polisi wa kimataifa –Interpol, kuwakamata wahusika.
Ubalozi wa Ukraine mjini Ankara imetaja meli zinazosafirisha chakula cha wizi kutoka Ukraine. Meli hizo ni Nadezhda, Finikia, Sormivskiy, Vera, na Mikhail Nenashev.
Ubalozu wa Ukraine mjini Beirut, umesema kwamba Russia imetuma tani 100,000 za ngano iliyoibwa kwa Syria, ambayo ni mshirika wake wa karibu.