Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 11:16

Russia yaahidi kupunguza mashambulizi yake karibu na mji mkuu wa Ukraine wa Kyiv.


Magari yaliyoharibiwa yaonekana mbele ya jengo lililoshambuliwa vikali katika mzozo kati ya Ukraine na Russia, katika mji wa kusini wenye bandari wa Mariupol, Machi 27, 2022. Picha ya Reuters.
Magari yaliyoharibiwa yaonekana mbele ya jengo lililoshambuliwa vikali katika mzozo kati ya Ukraine na Russia, katika mji wa kusini wenye bandari wa Mariupol, Machi 27, 2022. Picha ya Reuters.

Rais wa Marekani Joe Biden amesema Jumanne kwamba mataifa washirika ya magharibi yanasubiri kuona ikiwa Russia itatekeleza dhamira yake ya kupunguza mashambulizi karibu na mji mkuu wa Ukraine wa Kyiv na katika mji wa kaskazini wa Chernihiv.

“Tutaona kama watafanya walivyoahidi,” Biden amesema baada ya kuzungumza kwa simu na viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Italia.

“Inaonekana kuna makubaliano lakini wacha tuone kile walichoahidi kufanya.”

Biden ametoa matamshi hayo kwa waandishi wa habari kwenye White House baada ya jeshi la Russia kusema mapema Jumanne kwenye duru ya mazungumzo ya hivi karibuni nchini Uturuki kwamba, litapunguza operesheni zake karibu na Kyiv na Chernihiv.

Naibu waziri wa ulinzi wa Russia Alexander Fomin amesema hatua hiyo ni kutaka kuongeza uaminifu katika mazungumzo yenye lengo la kumaliza mapigano.

Vikosi vya Russia vilikwama kusonga mbele hivi karibuni kufuatia kujihami vikali kwa wapiganaji wa Ukraine.

Jumanne pia, waziri wa ulinzi wa Russia Sergei Shoigu amesema vikosi vya Russia vitajikita zaidi kwenye eneo la Donbas, ambalo linajumuisha majimbo yaliyojitenga ya Luhansk na Donetsk.

XS
SM
MD
LG