Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Juni 15, 2025 Local time: 14:26

Russia, Uturuki kushirikiana kuhusu nafaka zitakazopelekwa Afrika


Rais wa Uturuki Recep Tayipp Erdogan 9Kushoto) na mwenzake wa Russia Vladmir Putin (Kulia).
Rais wa Uturuki Recep Tayipp Erdogan 9Kushoto) na mwenzake wa Russia Vladmir Putin (Kulia).

Russia ilisema Jumatano kwamba Uturuki imekubali kimsingi, kushughulikia tani milioni moja za nafaka, ambazo Russia inapanga kutuma barani Afrika, kwa bei iliyopunguzwa, zikiwa zimenunuliwa  kwa msaada wa kifedha kutoka Qatar.

Moscow ilipendekeza mpango huo baada ya kuvunja mkataba ulioendelea kwa mwaka mmoja mwezi Julai, ambao uliiruhusu Ukraine kusafirisha nafaka kwa usalama kutoka bandari zake za bahari ya Black Sea, kwa matumaini ya kudhibiti kupanda kwa bei za vyakula duniani, kulikochochewa na uvamizi wa Russia.

Russia imekuwa ikizivutia nchi za Kiafrika, ambazo baadhi zimekuwa zikikabiliwa na uhaba wa chakula, kwa kuziahidi nafaka za bure au zilizopunguzwa bei - ingawa ni kiasi kidogo sana kuliko zile Ukraine imekuwa ikiuza nje.

"Makubaliano yote kimsingi yamefikiwa. Tunatarajia kwamba katika siku za usoni, tutaingia katika mawasiliano ya kufanya kazi, na pande zote, ili kushughulikia masuala yote ya kiufundi ya mpango kama huo," Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Alexander Grushko, aliwaambia waandishi wa habari, kwa mujibu wa shirika la habari la Russia, Interfax.

Kulingana na Moscow, Uturuki itashughulikia mauzo ya nje ya nafaka ya Russia lakini maelezo ya jukumu lake hayakuwa wazi.

Forum

XS
SM
MD
LG