Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 08:34

Riek Machar aondolewa mamlakani kama mkuu wa chama chake huko Sudan Kusini


Riek Machar, Makamu Rais wa Sudan Kusini
Riek Machar, Makamu Rais wa Sudan Kusini

Machar, mtu muhimu katika njia iliyopelekea umwagaji damu Sudan Kusini kuelekea uhuru na vita vya wenyewe kwa wenyewe aliondolewa madarakani kufuatia mkutano wa siku tatu wa viongozi wakuu wa SPLM/A-IO kaskazini mwa nchi hiyo mrengo wa chama hicho ulisema

Makamu wa Rais wa Sudan Kusini, Riek Machar ameondolewa mamlakani kama mkuu wa chama na majeshi yake, wanasema viongozi wapinzani ambao walimshutumu mwanasiasa huyo aliyegeuka kuwa muasi kwa kutowakilisha tena maslahi yao.

Machar, mtu muhimu katika njia iliyopelekea umwagaji damu Sudan Kusini kuelekea uhuru na vita vya wenyewe kwa wenyewe aliondolewa madarakani kufuatia mkutano wa siku tatu wa viongozi wakuu wa SPLM/A-IO kaskazini mwa nchi hiyo mrengo wa chama hicho ulisema.

Mkuu wa wafanyakazi wake, Luteni Jenerali wa kwanza Simon Gatwech Dual, alitangazwa kiongozi wa mpito wa kundi la upinzani ambalo linatawala nchi iliyokumbwa na matatizo katika ushirika wenye wasi wasi na maadui wa zamani.

XS
SM
MD
LG