Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 12:36

Ramaphosa apokea ripoti ya uchunguzi kuhusu ufisadi chini ya utawala wa Zuma


Rais Cyril Ramaphosa akitoa hotuba kuhusu kura ya bajeti ya ofisi ya rais katika bunge mjini Cape Town, June 9, 2022. Picha ya AFP
Rais Cyril Ramaphosa akitoa hotuba kuhusu kura ya bajeti ya ofisi ya rais katika bunge mjini Cape Town, June 9, 2022. Picha ya AFP

Matokeo ya mwisho ya uchunguzi wa miaka minne kuhusu ufisadi wa serikali nchini Afrika Kusini chini ya utawala wa Rais wa zamani Jacob Zuma yametangazwa Jumatano, na hivo kufungua njia kwa uchunguzi wa makosa ya jinai.

Akipokea ripoti ya uchunguzi huo, Rais Cyril Ramaphosa ameielezea rushwa kama “shambulio kwa demokrasia ya nchi.”

Ripoti hiyo imekabidhiwa kwa Ramaphosa kwenye ofisi yake mjini Pretoria na kiongozi wa jopo la uchunguzi na mwanasheria mkuu, Raymond Zondo, katika hafla iliyopeperushwa kwenye televisheni.

Uporaji na usimamizi mbovu wa mashirika ya serikali ya Afrika Kusini wakati wa miaka tisa ya Zuma madarakani umepewa jina la “utekaji wa serikali.”

“Ripoti hii inatupa fursa ya kuchukua hatua madhubuti kumaliza enzi ya utekaji wa serikali,” amesema Ramaphosa.

“Utekaji wa serikali hakika ulikuwa shambulio kwa demokrasia yetu. Unavunja haki ya kila mwanaume, kila mwanamke na kila mtoto nchini humu.”

XS
SM
MD
LG