Korona ambaye aliliongoza taifa hilo la Afrika Magharibi kuanzia 2007 hadi 2018, awali alihojiwa, mamlaka ikisema alikuwa mshukiwa rasmi katika mipango ya mapinduzi.
“Rais huyo wa zamani ameshitakiwa kwa makosa manne yakiwemo uhaini, makossa ya uhaini na kwa mashitaka mawili ya kuhifadhi,” taarifa iliyosainiwa na waziri wa habari Chernor Bah imesema.
Siku ya Jumanne Sierra Leone iliwafungulia mashitaka watu 12 kwa tuhuma za uhaini zinazohusiana na jaribio la mapinduzi akiwemo Amadu Koita, mwanajeshi wa zamani na mlinzi wa Koroma.
Koita alikuwa akifuatiliwa kwa kiasi kikubwa katika mitandao ya kijamii ambako amekuwa akiikosoa serikali ya sasa ya Rais Julius Maada Bio.
Novemba 26, washambuliaji wenye silaha walivamia ghala ya silaha kambi mbili za jeshi, magereza mawili, na vituo viwili vya polisi pamoja na kupambana na vikosi vya usalama.
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP
Forum