Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Julai 17, 2025 Local time: 06:55

Rais wa Uturuki aungwa mkono na mgombea aliyemnyima ushindi katika duru ya kwanza ya uchaguzi


Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akitoa hotuba kwenye makao makuu ya chama chake, mjini Ankara, Mei 15, 2023.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akitoa hotuba kwenye makao makuu ya chama chake, mjini Ankara, Mei 15, 2023.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan Jumatatu alipata uungwaji mkono wa mgombea wa mrengo mkali wa kiconservative ambaye nafasi yake ya tatu ilipelekea Uturuki kuandaa uchaguzi wa marudio kwa mara ya kwanza.

Asilimia 5.2 ya kura kwa Sinan Ogan katika uchaguzi mkuu wa Mei 14 ilisaidia kumnyima Erdogan ushindi mkubwa kwa mara ya kwanza katika utawala wake wa miaka 20.

Ogan alikutana na kiongozi huyo wa Uturuki siku ya Ijumaa na kufanya mazungumzo tofauti na washirika wa kiongozi wa upinzani Kemal Kilicdaroglu.

“Tutamuunga mkono mgombea wa chama cha the People’s Alliance, Recep Tayyip Erdogan, katika duru ya pili ya uchaguzi tarehe 28 Mei, aliwaambia waandishi wa habari.

Ogan anajitambulisha kama mfuasi sugu wa mrengo wa kihafidhina wa Uturuki uliopendekezwa na muanzilishi wa jamhuri ya baada ya ufalme wa Ottoman Mustafa Kemal Ataturk.

Aliomba mamilioni ya wahamiaji wafurushwe mara moja na kupendekeza msimamo thabiti dhidi ya magaidi, neno linalotumiwa dhidi ya makundi ya Wakurdi yanayopigania uhuru eneo la kusini mashariki mwa Uturuki.

XS
SM
MD
LG