Ofisi ya mpatanishi mkuu wa kitaifa imelitaja jaribio la Castillo la kuvunja bunge kama mapinduzi, ingawa mtaalam mmoja wa kisiasa ametofautiana na wazo hilo.
Eduardo Gamarra ambaye ni mtaalam wa sayansi ya siasa na pia mhadhiri kwenye chuo kikuu cha kimataifa cha Florida amesema kwamba bunge la Peru lina uwezo wa kumuondoa rais madarakani, wakati pia rais akiwa na uwezo wa kulivunja bunge, kwa hivyo hatua ya Castillo haikuwa mapinduzi.
Wabunge 101 dhidi ya 6 walipiga kura ya kuondolewa kwa Castillo kutoka ofisini kwa madai ya utovu wa maadili,wakati 10 hawakushiriki kupiga kura.
Facebook Forum