Uchunguzi ulioendeshwa na taasisi ya kupambana na ufisadi (ACB) kuhusu undanganyifu wa zabuni umehitimisha kuwa maafisa wa umma 53 wa sasa na wa zamani walipokea pesa kutoka kwa mfanyabiashara raia wa Uingereza mwenye asili ya Malawi Zuneth Sattar, kati ya mwezi Machi na Oktoba 2021, Chakwera amesema.
Sattar anafanyiwa uchunguzi nchini Uingereza na Malawi juu ya tuhuma za ufisadi, udanganyifu na utakatishaji wa fedha.
Kulingana na katiba ya Malawi, Chakwera hawezi kumsimamisha kazi au kumfukuza kazi Chilima kwa sababu ni afisa aliyechaguliwa.
βLa muhimu nachoweza kufanya kwa sasa, ni kumuweka kando na kumpokonya makujumu yote wakati nikisubiri taasisi ya kupambana na ufisadi ithibitishe tuhuma zinazomkabili,β amesema Chakwera.
Chilima hakutoa maelezo mara moja juu ya uamuzi huo. Alishirikiana na Chakwera kushinda uchaguzi wa rais wa 2020 katika muungano wa kupambana na ufisadi.
Katika hotuba kwa taifa, Chakwera alimfukuza kazi pia mkuu wa polisi George Kainja, ambaye alisikika kwenye mkanda uliorikodiwa akijadili mikataba na Sattar.