Taarifa za habari kutoka Ghana zinasema rais John Atta Mills amefariki dunia. Ofisi ya rais inasema kiongozi huyo aliyekuwa na umri wa miaka 68 alifariki ghafla leo masaa machache baada ya kuugua.Taarifa za habari za Ghana zinasema alifariki katika hospitali ya jeshi kwenye mji mkuu Accra. Hakuna maelezo ya haraka juu ya kifo chake.John Atta Mills aliongoza Ghana tangu mwaka 2009.
Ofisi ya rais nchini Ghana inasema amefariki katika hospitali ya jeshi mjini Accra.