Afrika Kusini katika miezi ya hivi karibuni ilikumbwa na moja ya mizozo mibaya ya nishati na kukatika kwa umeme kwa miaka mingi kumezidi kuwa mbaya zaidi.
Mgao wa umeme ulioratibiwa, umewekwa ili kusaidia mfumo wa umeme unaozalishwa na makaa ya mawe nchini humo uendelee kufanya kazi licha ya mahitaji makubwa.
Ramaphosa alikiri katika hotuba ya kila mwaka kuhusu hali ya taifa kwamba “ tuko katika mzozo mkubwa wa nishati.”
“Kwa hivyo tunatangaza janga la kitaifa kukabiliana na mzozo wa umeme na athari zake,” Ramaphosa alisema katika taarifa kuu ya hotuba yake ambayo ilicheleweshwa na wabunge wa upinzani ambao walijaribu kumzuia kuitoa.
Mtandao wa umeme, unaosimamiwa na kampuni ya nishati ya serikali ya Eskom, umeshindwa kuendana na mahitaji.
Facebook Forum