Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 01, 2023 Local time: 10:32

Rais Omar Al Bashir asema hawatarudi vitani


Wananchi wa Sudan Kusini wakionyesha uungaji mkono kura ya maoni katika mitaa ya Juba.

Licha ya mvutano kuongezeka Sudan rais Omar Al Bashir aahidi utulivu.

Rais wa Sudan Omar Al Bashir amesema nchi yake haitarudi tena vitani licha ya kuongezeka kwa mvutano kati ya kaskazini na kusini wakati kura ya uhuru wa kusini ikikaribia.

Vyombo vya habari vya serikali vilimkariri Bw. Bashir akisema kwamba serikali inafanya kazi kuweka utulivu kote nchini humo.

Kusini na kaskazini wamelaumiana kwa kuweka vikosi kwenye mpaka wao kabla ya kura ya maoni itakayofanyika January 9.

Mvutano ulizidi kuongezeka Jumanne wakati waziri wa ulinzi wa Sudan akisema kwamba huenda kura ya maoni ikacheleweshwa.

XS
SM
MD
LG