Mohamed Abdullahi Mohamed ambae ni maarufu kwa jina la “Farmajo” amechaguliwa kuwa Rais wa Somalia.
Rais aliye maliza muda wake Sheikh Mohamud amekubali kushindwa Jumatano baada ya raundi ya pili ya kura zilizopigwa na Bunge la Somalia huko Mogadishu.
Farmajo kabla ya hapo alikuwa waziri mkuu wa Somalia kati ya mwaka 2010 na 2011. Pia ni Raia wa Marekani ambae ameishi miaka mingi katika jiji la Buffalo, akifanya kazi katika serikali ya jimbo la New York.