Hatua hiyo inajumuisha mpango wa Deferred Enforced Departure DED, pamoja na Temporary Protected Status, TPS, ikiwa imechukuliwa kutokana na kuendelea kwa ghasia nchini mwao. Raia wa Lebanon ambao wameishi mfululizo hapa Marekani tangu Oktoba 16, 2023, wataruhusiwa kuomba hifadhi ya TPS.
Hata hivyo waliowasili baada ya ya tarehe hiyo hawatapewa stakabadhi hizo. Kamati inayopinga ubaguzi dhidi ya Waarabu, ADE imesifu hatua hiyo ya kulinda raia wa Lebanon dhidi ya vita vinavyoendelea, lakini imeomba Marekani kusitisha upelekaji wa silaha kwa Israel, ambazo zinatumika kushambulia Lebanon.
Mkurugenzi mkuu wa kitaifa wa Kamati hiyo Abed Ayoub, amasema kuwa kuhakikisha kuwa raia wa Lebanon waliopo Marekani hawalazimishwi kurudi kwenye hatari ni hatua ya kuridhisha. Hata hivyo amesema kuwa hatua bora zaidi ya kuchuliwa na utawala wa Biden ni kusitisha mara moja upelekaji wa silaha kwa Israel.
Forum