Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 01:58

Qatar inaandamwa na madai ya ukandamizaji wa haki za wafanyakazi waliojenga viwanja


Uwanja wa michezo wa Khalifa mjini Doha, utakaotumiwa kwa michuano ya kandanda, kombe la dunia. Okt 29 2022
Uwanja wa michezo wa Khalifa mjini Doha, utakaotumiwa kwa michuano ya kandanda, kombe la dunia. Okt 29 2022

Kundi la kutetea haki za kibinadamu limesema kwamba wafanyakazi kutoka nje ya Qatar, waliokuwa wanajesnga viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya kandanda ya kombe la dunia, walilazimishwa kufanya kazi katika mazingira magumu, kubaguliwa, kulipwa vibaya na kukumbana na dhuluma mbalimbali.

Ripoti ya kurasa 75 ya kundi la kutetea haki za binadamu, lenye makao yake mjini London, imetolewa wiki mbili kabla ya kuanza kwa mashindano ya kombe la dunia.

Wapenzi wa kandanda zaidi ya milioni 1.2 wanatarajiwa kuhudhuria mashindano hayo nchini Qatar.

Namrata Raju, mkurugenzi wa shirika la India la Equidem amesema kwamba wafuasi wa kandanda wanastahili kujua kuhusu matayarisho ya mashindano hayo.

"Mara nyingi, waajiri huwa wanachukua pasipoti za wafanyakazi kinyume cha sheria na sio tu nchini Qatar lakini katika nchi nyingi hatua ambayo kulingana na mfumo wa ufadhili wameanza kuleta mabadiliko. Lakini bado kuna pengo kubwa kwa kuzingatia yale wanayosema yamefanya kama mabadiliko katika sheria na yale wanayofanya."

Maafisa wa Qatar, wameshutumu wakosoaji kwamba wamekosa kutilia maanani mabadiliko yaliyofanywa na kwamba wana misimamo tofauti kuhusu taifa hilo la kwanza la kiarabu na la kiislamu kuandaa mashindano ya kandanda ya kombe la dunia.

Asilimia 95 ya wafanyakazi nchini Qatar ni raia kutoka nchi za nje.

Wamejenga viwanja na miundo msingi kwa kasi isiyo ya kawaida, baada ya Qatar kupata haki ya kuandaa mashindano hayo, mnamo mwaka 2010.

Miongoni mwa ujenzi huo ni viwanja vya michezo, mfumo wa reli ya mwendo wa kasi, barabara na hoteli.

XS
SM
MD
LG