Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 12:54

Putin asisitiza ujumbe wake kuelekea uchaguzi wa rais


Rais wa Russia, Vladimir Putin, Jumapili aliapa kuifanya Russia, kuwa huru na kujitegemea mbele ya nchi za Magharibi, katika hotuba yake ya kwanza ya kampeni kabla ya uchaguzi wa Machi na kuongeza muda wa utawala wake hadi mpaka 2030.

Putin atagombea muhula wa tano wa Kremlin, katika uchaguzi usio na upinzani wa kweli ambao utafanyika ikiwa ni zaidi ya miaka miwili tangu aanzishe mashambulizi ya uvamizi wa Ukraine.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 71 aliingia madarakani mwaka wa 2000, na kizazi kizima cha Russia cha sasa hakikumbuki maisha bila yeye.

Kura hiyo itaongeza muda wa utawala wake mpaka 2030 na kumpa uwezekano wa kukaa Kremlin mpaka mwaka 2036.

“Lazima tukumbuke na kamwe tusisahau na kuwaambia watoto wetu, Russia, itakuwa nchi huru inayojitosheleza,” Putin amesema wakati wa kongamano la chama tawala cha United Russia.

Forum

XS
SM
MD
LG