Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 14:28

Putin asikitishwa kutoalikwa kwa Russia, kumbukumbu ya NAZI


Rais wa Russian, Vladimir Putin.
Rais wa Russian, Vladimir Putin.

Rais wa Russia, Vladimir Putin, amesema kupuuza jukumu la Muungano wa Sovieti katika kukomboa kambi za kifo za Kinazi wa Wajerumani kama vile Auschwitz, na kutowaalika wanafamilia waliosalia wa wanajeshi wa Sovieti kwenye kumbukumbu za ukombozi ni kitendo cha aibu.

Kumbukumbu ya kuadhimisha miaka 80 tangu kukombolewa kwa kambi ya Auschwitz, nchini Poland kulikofanywa na wanajeshi wa Sovieti, ilihudhuriwa na Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy, Mfalme Charles wa Uingereza, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Rais wa Poland Andrzej Duda na viongozi wengine wengi.

Russia, mrithi wa Muungano wa Sovieti, haikualikwa kutokana na vita vya Ukraine.

“Hili ni jambo la kushangaza na la aibu,” Rais Putin amesema kupitia televisheni ya serikali ya Russia, katika mahojiano yaliyorushwa Jumapili.

Forum

XS
SM
MD
LG