Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 18:43

Puntland yatangaza sitisho la mapigano


Ramani ya Puntland, Somalia
Ramani ya Puntland, Somalia

Maafisa wa Somalia katika eneo lenye utawala kiasi la Puntland wametangaza kusimamisha mapigano kufuatia siku mbili za mapigano makali baina ya vikosi viwili vya usalama katika mji wa bandari ya biashara ya Bosaso.

Mapigano yalizuka Jumanne baina ya vikosi vya usalama vya Puntland, kitengo cha kukabiliana na ugaidi ambacho kilikuwa kinasaidiwa na Marekani, na vikosi vya kawaida vya usalama vya kikanda.

Takriban watu 14 waliuwawa na wengine 63 kujeruhiwa, kwa mujibu wa mashuhuda na vyanzo vya hospitali. Pande hizo zilijibizana kwa kufyatuliana risasi kwa kutumia bastola bunduki za rashasha na milipuko na kulazimisha wakazi kukimbia kwa mujibu wa shuhuda waliozungumza na VOA.

Waziri wa usalama wa eneo hilo Abdisamad Mohamed Galan ametangaza kusimamishwa mapigano Jumatano, akisema uamuzi huo ulifanywa baada ya viongozi wa kimila, wanazuoni, na viongozi wa kibiashara kuingilia kati.

XS
SM
MD
LG