Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 17:06

Polisi wa Kenya wamkamata mshukiwa mkuu wa shambulio dhidi ya mwanadiplomasia wa kike.


Dereva wa boda boda akionekana mjini kati Nairobi, wakati wa msongamano wa magari nyakati za jioni. Septemba 26, 2018. Picha ya AFP.
Dereva wa boda boda akionekana mjini kati Nairobi, wakati wa msongamano wa magari nyakati za jioni. Septemba 26, 2018. Picha ya AFP.

Polisi wa Kenya wamesema Jumatatu kwamba wamemkamata mshukiwa mkuu wa shambulio dhidi ya mwanadiplomasia wa kike, ambalo lilizua gumzo na maandamano katika taifa hilo la Afrika mashariki.

Mwanamke huyo alishambuliwa mchana kweupe na kundi ka waendesha boda boda baada ya ajali ya barabarani mapema mwezi huu, polisi walisema.

Waendesha boda boda 16 walikamatwa wiki iliyopita baada ya video iliyotanda kwenye mitandao ya kijamii ikiwaonyesha wanaume hao, wakirarua nguo za mwanamke huyo, huku akipiga kelele za kuomba msaada akiwa ndani ya gari lake na kulazimishwa kufungua mlango wa gari hilo.

Lakini anayedaiwa kuwa kiongozi wa shambulio hilo alitoroka kupitia mfereji wa maji taka na kukwepa kukamatwa hadi Jumatatu, alipotiwa mbaroni katika mji ulio karibu na mpaka wa Tanzania, takriban kilomita 430 kaskazini magharibi mwa Nairobi.

Polisi wamesema “ walimvamia alipojaribu kuvuka mpaka” na kusema kwamba atasafirishwa kwa ndege hadi Nairobi, “ambako atakabiliwa na mkono wa sheria”.

XS
SM
MD
LG