Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Desemba 08, 2023 Local time: 04:55

Polisi wa Denmark na Sweden wazuia shambulizi


Polisi huko magharibi mwa Copehagen, baada ya shirika la ujasusi la Denmark kukamata watu wanne wanaoshukiwa kupanga shambulizi la kigaidi.
(AP Photo/Polfoto/Jens Dresling).
Polisi huko magharibi mwa Copehagen, baada ya shirika la ujasusi la Denmark kukamata watu wanne wanaoshukiwa kupanga shambulizi la kigaidi. (AP Photo/Polfoto/Jens Dresling).

Polisi wa Denmark na Sweden wanasema wamezuia shambulizi la kigaidi jumatano muda mfupi kabla ya kutokea huko Copenhagen na kukamata watu watano ambao walikuwa wamepanga kufanya mauaji ya halaiki.

Shirika la ujasusi la Denmark linasema wanachama wa kundi la wanamgambo wa kiislam wenye msimamo mkali walijaribu kulazimisha kuingia kwenye ofisi za gazeti moja la kila siku la Jyllands Posten na kuuwa watu wengi iwezekanavyo.

Gazeti hilo liliwakasirisha waislam mwaka 2005 kwa kuchora katuni za mtume Muhamad.

Washukiwa wanne kati yao walikamatwa huko Copenhagen. Mtu wa tano alikamatwa Sweden.

XS
SM
MD
LG