Marekani ilijiondoa mwaka 2018 ikilalamika kuhusu msimamo dhidi ya Israeli na utawala mbaya katika shirika hilo.
Kabla ya kujiondoa, Marekani ilikuwa ni mfadhili pekee mkubwa zaidi wa UNESCO, ikitoa takriban moja ya tano ya ufadhili wote kwa shirika hilo.
Maafisa wa Marekani walisema mapema mwezi huu kuwa shauku yao ya kurejea UNESCO ilichochewa na wasiwasi kuhusu ushawishi wa China katika uwekaji wa sera kwenye shirika hilo, hususan zile za akili bandia (artificial intelligence) na mafunzo ya teknolojia.
Kama sehemu ya pendekezo la mpango wa kurejea katika shirika hilo, utawala wa Biden umeomba dola za Kimarekani milioni 150 kwa ajili ya ufadhili wa michango na madeni yake kwa UNESCO.
Baadhi ya taarifa katika ripoti hii zinatokana na mashirika ya habari ya AP na Reuters.
Forum