IMF katikati ya mwezi wa Juni ilieleza kutoridhishwa na bajeti ya awali ya nchi hiyo, ikisema imeshindwa kupanua wigo wa kodi kwa njia ya kimaendeleo zaidi.
Bajeti iliyorekebishwa iliidhinishwa siku moja baada ya waziri wa fedha Ishaq Dar, kuwasilisha kodi mpya na kupunguza matumizi.
“Muswada wa fedha umepitishwa,” spika wa bunge Raja Pervaiz Ashraf, alisema katika matangazo ya moja kwa moja ya televisheni siku ya Jumapili.
Huku akiba ya fedha haitoshi kugharamia uagizaji wa bidhaa kwa mwezi mmoja, Pakistan inakabiliwa na mzozo mkubwa wa malipo, ambao wachambuzi wanasema huenda ukaingia katika hali ya kutolipa deni ikiwa fedha za IMF hazitafanikiwa.
Forum